Thursday, April 5, 2012

Kilimanjaro yatangaza siku ya kutoa Tuzo na Kiingilio

Kampuni ya Bi Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Kiliminjaro Prenium Lager kwa kushirikiana na baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) leo wametangaza rasmi tarehe ya usiku wa kutoa Tuzo za Muziki Tanzania (Kilimanjaro Tanzania Music Award)
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam,Meneja wa bia ya Kilimanjari Bwana George Kavishe alisema tarehe ya siku ya kutoa tuzo hizo ni tarehe 12 april 2012 ndani ya ukumbi wa Mlimani City.
“Shughuli itaanza rasmi saa moja jioni ikipambwa na burudani safi ilipangwa kwa umahili na mtaalam kutoka nyumbani. Wanaii watao panda usiku wa kutoa tuzo ni pamoja na Diamond, kundi zima la Tmk Wanaume, Charles Baba, Kharid Chokoraa, Recho, Ommy Dimpozi, Bichuka na wengine” alisema Kavishe.
Aliendelea kusema, tamasha litakuwa kali kwani sio tu waitaimba nyimbo zao lakini wataimba na nyimbo za zamani zilizowahikutamba za kwao pamoja na wanamuziki nguli nchini.
Pia meneja wa Kilimanjaro ametoa shukrani kwa Watanzania  kwa kujitokeza kwa wingi katika zoezi la kupiga kura .
“Tumevuka lengola idadi ya kura kwa Nyanja zote ni maana ya ujumbe mfupi wa simu, vipeperushi, barua pepe na mitandao hii imaanisha Tuzo za zimekubalika na zimepokelea na jamii”
Aidha aliendeleakutoa shukrani kwa BASATA kwa kuendelea kutoaushirikiano na bia ya Kilimanjaro na kuipatia tena kibali cha kudhamini na kuendeleza shughuli za  Tuzo za Muziki Tanzania.
Tiketi zitauzwa kwa kwa VIP shilingi elfu 75 ikijumuishwa na chakula cha jioni (Buffet) na vinywaji bulena kawaida kwa shilingi elfu 20, na bia moja ya bule.
Tiketi zitauzwa maeneo ya Ukumbi wa Mlimani City kuanzia jumatatu,  Posta  Mpya ‘Baraka Golden mtaa wa Azikiwe nyuma ya CRDB  Bank’, Zizzou Fashion ya Victoria, Sinza na Tegeta, Bornie To Shine Mwenge, Robby One Fashen Kinondoni, Engine Petrol station Mbezi.
mwisho